Monday, January 28, 2013

GRELLA ATUNDIKA DARUGA.

KIUNGO wa kimataifa wa Australia, Vince Grella ambaye pia amewahi kucheza katika vilabu vya Blackburn Rovers na Parma katika miaka 17 alioyocheza soka ameamua kustaafu mchezo huo baada ya kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara. Grella mwenye umri wa miaka 33 alitangaza uamuzi huo mapema leo ikiwa ni siku mbili baada ya kuumia katika mchezo wake wa kwanza na klabu yake mpya ya Melbourne Heart inayoshiriki Ligi Kuu nchini Australia maarufu kama A-League. Akitangaza uamuzi huo Grella amesema anaona miaka 17 aliyocheza soka inatosha kwakuwa mwili wake hivi sasa hauwezi kukabiliana na mikiki ya uwanjani. Grella alikuwemo katika kikosi cha timu ya taifa ya Australia ambacho kilishirikisho michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani na 2010 nchini Afrika Kusini na kucheza michezo 46 ya kimataifa. Kwa upande wa vilabu nyota huyo aliwahi kucheza katika vilabu vya Parma, Empoli na Torino zote za Italia kabla ya kutimkia Uingereza katika klabu ya Blackburn ambayo aliondoka mwaka jana.

No comments:

Post a Comment