Monday, January 28, 2013

AFCON 2013: MWAMUZI AFUNGASHIWA VIRAGO.

MWAMUZI kutoka Misri ambaye alichezesha mchezo wa kundi C kati ya Nigeria na Zambia Ijumaa iliyopita katika Uwanja wa Mbombela jijini Nelspruit, Gehad Grisha ameondolewa kuchezesha mechi zingine za michuano hiyo inayoendelea nchini Afrika Kusini. Grisha aliwapatia penati yenye utata Zambia katika dakika za majeruhi za mchezo baina ya timu hizo kitendo ambacho kilipelekea kuamsha hasira za wachezaji na viongozi waliokuwepo katika benchi la ufundi. Shirikisho la Soka la Nigeria-NFF liliwasilisha malalamiko yao mbele ya Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF kuhusu suala la mwamuzi huyo. CAF ilithibitisha kumuondoa Grisha kwenye orodha ya waamuzi wake baada ya kufanyia uchunguzi suala hilo na kugundua makosa aliyofanya kwenye mchezo huo. Nigeria inahitaji ushindi katika mchezo wake wa kesho utakaofanyika jijini Rustenburg dhidi ya Ethiopia ili kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment