Tuesday, January 22, 2013

AFCON 2013: KESHI ATEGEMEA KUMTUMIA MOSES IJUMAA.

NIGERIA inamatarajio kuwa winga wake anayecheza katika klabu ya Chelsea ya Uingereza, Victor Moses atakuwa amepona goti kwa wakati kabla ya mchezo wao wa Ijumaa dhidi ya mabingwa watetezi wa michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon Zambia. Moses hakuwemo katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kilitoa sare ya bao 1-1 na Burkina Faso kwasababu ya kujiuguza goti lake na nafasi yake kuchukuliwa na mshambuliaji wa Dynamo Kiev ya Ukraine Brown Ideye. Kocha wa Nigeria Stephen Keshi amesema alimwacha kumtumia Moses kuhofia kujitonesha tena lakini ana matumaini winga huyo atakuwa fiti kwa ajili ya mchezo dhidi ya Zambia. Beki Efe Ambrose anayecheza klabu ya Celtic Glasgow ataukosa mchezo wa Ijumaa baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Burkina Faso na nafasi yake inategemewa kuchuliwa na Kenneth Omeruo. 

No comments:

Post a Comment