Tuesday, January 22, 2013

NITASTAAFU NIKIWA BARCELONA - INIESTA.

KIUNGO nyota wa kimataifa wa Hispania na klabu ya Barcelona, Andres Iniesta amebainisha kuwa hana mpango ya kuondoka katika klabu hiyo na kudai kuwa anataka kutundika daruga akiwa hapo. Iniesta mwenye umri wa miaka 28 ameshacheza mechi zaidi ya 400 katika kikosi cha kwanza cha Barcelona toka alipotoka katika shule ya klabu hiyo na anategemea kuendelea kuwepo zaidi hapo. Akihojiwa Iniesta amesema nia yake ni kucheza mpaka atapostaafu akiwa katika klabu hiyo na kitu pekee kinachoweza kubadilisha ni kiwango chake kwani kama kitashuka na klabu kuamua kumuacha ndio anayoweza kuondoka. Nyota pia alikiri kuwa timu hiyo inakabiliwa na wakati mgumu hivi sasa na wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanarejea katika kiwango chao haraka kabla ya mchezo wa Kombe la Mfalme dhidi ya Malaga.

No comments:

Post a Comment