Tuesday, January 22, 2013

PLATINI AMPONGEZA PRINCE BOATENG.

RAIS wa Shirikisho la Soka arani Ulaya, Michel Platini ametofautiana na rais wa Shirikisho la Soka la Dunia Sepp Blatter kuhusu suala la Kevin-Prince Boateng kuwaongoza wachezaji wenzake wa AC Milan kutoka uwanjani baada ya kufanyiwa vitendo vya kibaguzi mapema mwezi huu. Blatter amesema wachezaji hawapaswi kujichukuliwa sheria mkononi ingawa alidai kuwa mashabiki wanaokutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo wanapaswa kuchuliwa hatua aidha kwa klabu kukatwa alama au kufungiwa kabisa. Hatahivyo, Platini aliiambia radio moja nchini Ufaransa kuwa anakiunga mkono kitendo kilichofanywa na nyota huyo wa kimataifa kutoka Ghana kwani tatizo hilo linaonekana kuota mizizi katika siku za karibuni. Platini mwenye umri wa miaka 57 amesema ulikuwa ni uamuzi wa kishujaa uliofanywa na wachezaji wa Milan na baada ya tukio hilo aliwapigia simu na kuwapongeza.

No comments:

Post a Comment