Tuesday, January 22, 2013

AUSTRALIA OPEN: FERRER, SHARAPOVA WATINGA NUSU FAINALI.

MCHEZAJI nyota wa tenisi anayeshika namba nne katika orodha za ubora duniani David Ferrer amefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya wazi ya Australia baada ya kumfunga Mhispania mwenzake Nicolas Almagro katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Rod Laver Arena jijini Melbourne. Katika mchezo huo Ferrer ilibidi apambane kiume baada ya kuwa nyuma kwa seti mbili na kufanikiwa kumfunga Almagro kwa 4-6 4-6 7-5 7-6 6-2 ambapo sasa anatarajia kukutana na aidha Novak Djokovic au Tomas Berdych katika hatua ya nusu fainali. Kwa upande wa wanawake mwanadada Maria Sharapova aayeshika namba mbili katika orodha za ubora naye alifanikiwa kutinga nusu fainali baada ya kumuondosha Mrusi mwenzake Ekaterina Makarova. Sharapova sasa atachuana na Li Na wa China ambaye naye alitinga hatua hiyo baada ya kumsambaratisha Agnieszka Radwanska.

No comments:

Post a Comment