Monday, January 21, 2013

AUSTRALIA OPEN: FEDERER, MURRAY WATINGA ROBO FAINALI.

WACHEZAJI nyota wa mchezo wa tenisi, Roger Federer anayeshika namba mbili katika orodha za ubora duniani na Andy Murray anayeshika namba tatu wameonyesha ubora wao kwa kutinga robo fainali ya michuano ya wazi Australia. Federer raia Switzerland alifanikiwa kutinga hatu hiyo baada ya kumfunga Milos Raonic wa Canada kwa 6-4 7-6 6-2 akitumia muda wa saa moja na dakika 53 wakati Murray alimsambaratisha Gilles Simon wa Ufaransa kwa 6-3 6-1 6-3 akitumia muda wa saa moja na dakika 35. Murray sasa takutana na Jeremy Chardy katika hatua ya robo fainali wakati Federer atapambana na Jo-Wilfried Tsonga katika hatua ya robo fainali. Kwa upande wa wanawake bingwa mtetezi wa michuano hiyo Victoria Azarenka ametinga hatua ya robo fainali baada ya kumfunga kirahisi Elena Vesnina na kujiweeka katika nafasi nzuri ya kukwaana na Serena Williams katika hatua ya nusu fainali. Azarenka alimfunga Vesnina kirahisi kwa 6-1 6-1 na kukata tiketi ya robo fainali ambayo atacheza na Svetlana Kuznetsova wakati Williams ambaye anaonekana yuko katika kiwango bora alimsambaratisha Maria Kirilenko kwa 6-2 6-0 na kutinga hatua hiyo. 

No comments:

Post a Comment