Monday, January 21, 2013

GALATASARAY YAMNASA SNEIJDER, MILAN YAMNYATIA KAKA.

KLABU ya Galatasaray imedai kuwa imemnasa kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Uholanzi, Wesley Sneijder kwa ada euro milioni 7.5 kutoka klabu ya Inter Milan ya Italia. Galatasaray yenye maskani yake nchini Uturuki imesema kuwa imesainisha nyota huuyo mkataba wenye thamani ya euro milioni kwa mwaka mpaka mwaka 2016 baada ya kushindwa kuafikiana suala la malipo na Inter. Sneijder alijiunga na Inter akitokea Madrid mwaka 2009 na kuisaidia klabu hiyo kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Serie A na Kombe la Italia mwaka 2010. Wakati pazia la usajili wa dirisha dogo likielekea kufungwa Januari 31, klabu ya AC Milan ya Italia imepanga kumrejesha kiungo wake wa zamani wa kimataifa wa Brazil Kaka kutokea Madrid. Kaka mwenye umri wa miaka 30 aliondoka Milan mwaka 2009 baada ya misimu sita katika klabu hiyo na kushinda mataji ya Serie A, Ligi ya Mabingwa Ulaya na Klabu Bingwa ya Dunia.

No comments:

Post a Comment