Monday, January 21, 2013

FALACAO NJE WIKI TATU.

MATARAJIO madogo ya kuwafikia vinara wa Ligi Kuu nchini Hispania Barcelona, waliyokuwanayo Atletico Madrid yaliingia katika kikwazo Jumapili baada ya mshambuliaji wake tegemeo Radamel Falcao kupata majeruhi ya mguu ambayo yatamuweka nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki tatu akijiuguza. Falcao alianza kuchechea wakati akikokota mpira na mara moja aliomba kutolewa katika dakika ya 57 wakati Atletico ilipopata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Levante na kupunguza pengo la alama na Barcelona ambao walifungwa mchezo wao wa Jumamosi dhidi ya Real Sociedad. Meneja wa Atletico Diego Simeone alithibitisha kuumia kwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Colombia na kudai kuwa anaweza kukaa kwa siku 20 au zaidi. Falcao ameifungia Atletico mabao 18 msimu huu na kuisaidia timu hiyo kukaa katika nafasi ya pili wakiwa alama nyuma ya Barcelona.

No comments:

Post a Comment