Sunday, January 27, 2013

CITY YAPATA PIGO.

BEKI wa Manchester City, Vincent Kompany anatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi ya Queens Park Rangers-QPR baada ya kuumia katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Stoke City ambao walishinda kwa bao 1-0. Kocha msaidizi wa City David Platt amesema ni mapema mno kujua mchezaji huyo atakaa nje muda gani lakini mchezo wa Jumanne dhidi ya QPR lazima ataukosa. Kompany alilazimika kutolewa nje kwa kuumia baada ya nusu saa katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Britannia ambapo taarifa zaidi juu ya hilo zitatolewa baadae baada ya kufanyiwa vipimo vya afya kuchunguza ukubwa wa tatizo. Kuumia kwa Kompany ambaye ni beki wa kati kutakuwa pigo kubwa kwa klabu hiyo ambayo tayari imemkosa nyota wake anayeweza kucheza katika nafasi hiyo YayaToure ambaye yuko na timu yake ya taifa Ivory Coast katika michuano ya Mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment