Sunday, January 27, 2013

ILIKUWA NI KAMA KAMARI - WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekiri kuwa kuwapumzisha baadhi ya nyota wake katika mchezo wa mzunguko wa nne wa Kombe la FA dhidi ya Brighton ilikuwa ni kama kucheza kamari ambayo angeweza kushindwa. Kikosi cha Wenger ambacho kilikuwa kikicheza ugenini katika Uwanja wa Amex iliwapumzisha nyota wake Theo Walcott, Jack Wilshere na Santi Cazorla kuanza katika kikosi cha kwanza. Lakini kocha huyo ilibidi aongeze nguvu katika kipindi cha pili kwa kumuingiza Walcott ambaye alifunga bao na kuipeleka timu hiyo katika mzunguko wa tano wa michuano hiyo kwa ushindi wa mabao 3-2. Wenger alidai kuwa kiendo cha kubadilisha wachezaji na kuwapumzisha wengine kilikuwa ni kama kamari ambapo kama angeshindwa angelaumiwa kwa maamuzi mabovu aliyochukua lakini bahati nzuri haikutokea hivyo. Arsenal iko katika harakati za kusaka taji lao la kwanza baada ya kupita miaka nane bila kuambulia chochote.

No comments:

Post a Comment