Sunday, January 27, 2013

JUVENTUS YAMSAJILI ANELKA.

RAIS wa klabu ya Juventus ya Italia, Beppe Moratta amesema wamemsainisha mkataba wa miezi mitano mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Nicolas Anelka kutoka klabu ya Shanghai Shenhua ya China. Anelka mwenye umri wa miaka 33 anakuwa mchezaji wa pili mwenye jina kubwa kusajiliwa na mabingwa hao wa Serie A ndani ya wiki moja baada ya klabu hiyo pia kumnyakuwa nyota wa kimataifa wa Hispania Fernando Llorente ambaye atajiunga na klabu hiyo Julai 1 mwaka huu. Moratta amesema Juventus walikuwa wakihitaji kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji ambayo imepwaya ndio maana wakaamua kumsajili Anelka na kama akifanya vizuri mwishoni mwa msimu wanaweza kufikiria kumuongeza muda mwingine. Anelka ambaye alianza kucheza soka katika klabu ya Paris Saint-Germain-PSG ya Ufaransa na abaadae kucheza katika vilabu vya Arsenal, Real Madrid na Chelsea kabla ya kuondoka kwenda Shanghai ambapo kuna tetesi kuwa amechoshwa na maisha ya klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment