Sunday, January 27, 2013

WACHEZAJI WAWILI WAPOTEZA MAISHA VURUGU ZA PORT SAID.

WADAU wa soka nchini Misri wako katika maombolezo baada ya mchezaji wa Marek Mahmoud Abd Al Halem na golikipa wa zamani wa Al Masry Tamer Fahalawas kuuwawa katika vurugu zinazoendelea huko Port Said. Watu zaidi ya 30 wameuliwa Port Said kuanzia Jumamosi katika mapigano waandamanaji na vikosi vya usalama vya eneo hilo vurugu ambazo zilizuka baada ya Mahakama nchini humo kuwahukumu kifo watu 21 ambao walihusika katika vurugu ziliouwa watu 74 katika mchezo wa soka kati ya Al Masry na Al Ahly. Mashabiki wa timu zote mbili ambao wanajulikana kama Ultras wanadai kuwa polisi nao walihusika kwa kiasi kuchangia vifi vilivyotokea Port Said na kumlaumu rais wa Misri Mohammed Morsi kwa kushindwa kulisuka upya jeshi hilo. Mwenyekiti wa Merekh Morsy Sarhan alithibitisha kifo cha Abd Al Halem ambaye alijunga na timu hiyo miezi michache iliyopita ambapo tukio hilo lilimkuta wakati akielekea mazoezini. Sarhan aliongeza kuwa wataomboleza kifi cha mchezaji huyo kwa siku tatu ambaye alipigwa risasi pamoja na kutokuwa na hatia na kuwataka watu kuheshimu maamuzi ya mahakama ili maisha ya mchezo wa soka nchini humo yarejee kama kawaida.

No comments:

Post a Comment