Sunday, February 17, 2013

ALVES ASIFU KIWANGO CHA MESSI.

BEKI wa klabu ya Barcelona, Dani Alves amesifu kiwango cha mshabuliaji nyota wa klabu hyo Lionel Messi kwa kudai kuwa hufanya kazi yao kuwa rahisi pindi awapo uwanjani. Alves alijiunga katika orodha ya watu wengi waliosifia kiwango cha nyota huyo wa kimataifa wa Argentina baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 2-1 waliopata ugenini dhidi ya Granada. Messi alifunga bao lake la 300 na 301 kwa klabu hiyo baada ya kuwa nyuma kwa bao lililofungwa katika kipindi cha kwanza na kufanikiwa kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga. Alves amesema kucheza na Messi kwenye timu moja kunafanya mambo yawe rahisi zaidi kutokana na kiwango cha hali ya juu alichonacho nyota huyo hivyo kufanya matokeo kuwa mazuri baada ya dakika 90. Messi amefikisha mabao 37 katika ligi msimu huu huku wakitofautiana kwa alama 15 na Atletico Madrid ambao wanashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo. 

No comments:

Post a Comment