Sunday, February 17, 2013

VILANOVA YUKO KATIKA HALI NZURI - ZUBIZARRETA.

MKURUGENZI wa Michezo wa klabu ya Barcelona, Andoni Zubizarreta amesema kuwa meneja wa klabu hiyo Tito Vilanova yuko katika hali nzuri toka lianza matibabu yake huko jijini New York, Marekani. Zubizarreta alibainisha kuwa matibabu ya mionzi ili kutibu kansa ya koo inayomkabili Vilanova yanaendelea vyema na hivi karibuni anaweza kurejea kuendelea na kibarua chake kama kawaida. Vilanova mwenye umri wa miaka 44 alichukua kibarua cha kukinoa kikosi cha Barcelona katika kipindi ca majira ya kiangazi lakini kabla ya nusu ya msimu aligundulika kuwa na kansa ya tezi ambayo hivi anapatiwa matibabu yake huko New York. Zubizarreta amesema kocha huyo kwasasa amerejea katika hali yake ya kawaida baada ya mionzi huku akitizama soka katika luninga kila Barcelona inapokuwa uwanjani na anashukuru watu wote wanaomuombe katika kipindi hiki kigumu.

No comments:

Post a Comment