Sunday, February 17, 2013

SABC YAJITETEA KUONYESHA KIPINDI CHA STEENKAMP.

TELEVISHENI ya SABC ya nchini Afrika Kusini imetetea uamuzi wake wa kuonyesha kipindi kilichorekodia na Reeva Steenkamp, rafiki wa kike wa mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius ambaye anatuhumiwa kumuua mwanadada huyo. Muandaaji wa kipindi hicho, Samantha Moon aliliambia shirika la habari a BBC kuwa uamuzi wa kuonyesha kipindi hicho ulikuja baada ya kushauriana na familia ya mwanadada huyo ambaye aliwahi kuwa mwanamitindo. Kipindi hicho kiitwacho Tropika Island Treasure kilirekodiwa nchini Jamaica ambapo watu kadhaa hushindanishwa kugombea zawadi ya dola 113,500. Kwa upande mwingine mjomba wa Pistorius amesema jana kuwa mwanariadha huyo ambaye aliweka historia mwaka jana kwa kushiriki katika olimpiki ya watu wa kawaida pamoja na ile ya walemavu bado yuko katika mshituko na masikitiko makubwa kutokana na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment