Monday, February 18, 2013

MTANIKUMBUKA NIKIONDOKA - WENGER

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amewaonya mashabiki wa klabu hiyo wanaomponda kwamba watamkumbuka wakati akiwa ameondoka. Akizungumza kabla ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich Wenger alitetea rekodi yake toka aanze kuinoa klabu hiyo na kuwahakikishia kuwa lazima watamkumbuka wakati ataoondoka. Wenger alidai kuwa amekuwa akifundisha soka kwa kipindi cha miaka 30 na miaka 16 kati ya hiyo amefanya kazi Uingereza hivyo anastahili heshima kutokana na mafanikio mengi ambayo ameipa Arsenal katika kipindi chote. Katika kipindi cha karibuni Wenger amekataa kazi ya Kuzinoa timu za taifa za Uingereza, Ufaransa pamoja na klabu za Bayern Munich, Real Madrid na Paris Saint-Germain ambazo zote zilikuwa zikimuwania kutaka huduma yake. Baadhi ya mashabiki wa Arsenal wameonyesha kuishiwa na imani na kocha huyo baada ya miaka nane kupita bila ya kushinda taji lolote huku mara ya mwisho kufanya hivyo ikiwa ni mwaka 2005 waliponyakuwa Kombe la FA.

No comments:

Post a Comment