Monday, February 18, 2013

CITY WAANZA MBIO ZA KUMGOMBEA NEYMAR.

KLABU ya Manchester City yenye nguvu kubwa kifedha katika Ligi Kuu nchini Uingereza wamepiga hatua yao ya kwanza katika mbio za kumuwania mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Brazil, Neymar. Maofisa wa ngazi za juu wa klabu hiyo Ferran Soriano na Txiki Begiristain wametajwa kuanza mazungumzo ya awali na familia pamoja na mwakilishi wa nyota huyo katika Uwanja wa Wembley wakati wa mchezo wa kirafiki kati ya Uingereza na Brazil uliochezwa Februari 6 mwaka huu. Ofisa Mkuu Soriano na Begiristain ambaye ni mkurugenzi wa soka wa klabu hiyo walikuwa wageni waalikwa wa Chama cha Soka cha Uingereza-FA katika mchezo huo. Katika mchezo huo ambao Neymar hakung’ara sana baada ya Uingereza kushinda kwa mabao 2-1 maofisa hao walionekana wakijongea karibu na mahali familia ya Neymar ilipokuwa imekaa huku mara kwa mara wakiwa katika mazungumzo na baba wa nyota huyo.

No comments:

Post a Comment