Monday, February 18, 2013

TUKIKUBALI KUFUNGWA SAN SIRO TUMENG'OKA - BOJAN.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Barcelona, Bojan Krkic anaamini kuwa kufungwa kwa klabu yake ya sasa ya AC Milan katika mchezo wa kwanza wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kutakuwa kumefifisha matumaini yao ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo. Nyota huyo alielezea umuhimu wa Milan kuepuka kufungwa katika mchezo wa kesho usiku ambao wataikaribisha Barcelona katika uwanja wao wa nyumbani wa San Siro. Bojan amesema watakuwa wakicheza na timu bora duniani lakini wanashukuru kwakuwa wenyewe watakuwa na mashabiki watakaokuwa nyuma yao ambapo wanachotakiwa kufanya ni kupata angalau sare ili kuweka matumaini yao hai kwa mchezo wa marudiano. Bajan mwenye umri wa miaka 22 aliondoka Barcelona mwaka 2011 na kubainisha kuwa bado anawasiliana na wachezaji wenzake wa zamani ambao walimsaidia kwa namna moja au nyingine kufikia hapo alipo.

No comments:

Post a Comment