Thursday, February 21, 2013

DEL PIERO AONGEZA MKATABA SYDNEY.

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa kimataifa wa Italia na klabu ya Juventus, Alessandro Del Piero amesaini mkataba mwingine wa msimu mmoja katika klabu ya Sydney FC inayoshiriki Ligi Kuu nchini Australia maarufu kama A-League. Del Piero mwenye umri wa miaka 38 alitangaza uamuzi wake huo leo kabla ya muda wa klabu hiyo kufanya mkutano wa waandishi habari. Nyota huyo ambaye alijunga na Sydney msimu wa 2012-2013 ameshafunga mabao 11 katika mechi 18 za A-League alizocheza na tayari ameshaweka rekodi katika klabu hiyo kwa kufunga mabao mengi zaidi katika mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo. Mwenyekiti wa Sydney Scott Barlow amesifu wazo la kumsajili nyota huyo kwamba lilikuwa sahihi kwani hajawaangusha na amekuwa akionyesha kiwango bora zaidi kadri siku zinavyozidi kusonga mbele.

No comments:

Post a Comment