Thursday, February 21, 2013

WAKALA WA NEYMAR AMSHAMBULIA PELE.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa Brazil Neymar amesema kuwa shutuma za hivi karibuni alizotoa nguli wa soka wa nchi hiyo Pele kwa nyota huyo zinatokana na wivu. Wakala huyo alidai kuwa Pele angekuwa mchezaji dhaifu katika kikosi cha nyota wa Brazil kama angekuwa anacheza kipindi hiki baada ya nguli huyo ambaye amenyakuwa Kombe la Dunia mara tatu akiwa na kikosi cha nchi hiyo, kuponda kiwango cha Neymar kwenye timu ya taifa. Wakala wa nyota huyo aliendelea kurusha makombora kwa Pele akidai kuwa kama nguli huyo angekuwa akicheza katika miaka ya hivi sasa asingeweza kumfikia kiwango cha Neymar kwasababu mabeki kipindi hicho walikuwa wanacheza taratibu tofauti na hivi sasa. Ni mwaka mmoja uliopita ambapo Pele mwenye umri wamiaka 72 alimsifia nyota huyo kwamba ni moja wa wachezaji bora kabisa duniani lakini heshima hiyo inaonekana kutetereka kati ya wawili hao baada ya shutuma alizotoa pele karibuni.

No comments:

Post a Comment