Thursday, February 21, 2013

MASHABIKI TOTTENHAM WASHAMBULIWA UFARANSA.

MASHABIKI wa klabu ya Tottenham Hotspurs wameshambuliwa katika bar huko jijini Lyon nchini Ufaransa kabla ya mchezo wao wa Europa League dhidi ya Olympique Lyon utakaochezwa baadae leo. Mashabiki watatu walikimbizwa hospitali baada ya kundi la watu kuvamia na kuvunja madirisha ya vioo katika bar hiyo ambapo mashabiki wengine wakiumizwa na vioo vilivyokuwa vikiruka. Ofisa wa mambo ya nje alithibitisha kuwa wanalifanyia uchunguzi tukio ambalo limetokea saa 24 kabla ya mtanange baina ya timu hizo katika hatua ya timu 32 bora kwenye michuano hiyo. Katika mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Uingereza katika Uwanja wa White Hart Lane Alhamisi iliyopita Tottenham walifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1. 

No comments:

Post a Comment