Friday, February 22, 2013

HATUKUCHEZA VIBAYA SANA - XAVI.

KIUNGO nyota wa klabu ya Barcelona, Xavi Hernandez amekataa kuwa kipigo cha mabao 2-0 walichokipata kutoka kwa AC Milan Jumatano iliyopita kilitokana na kucheza kwa kiwango kibovu kabisa toka msimu umeanza. Kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania ni mchezaji pekee wa Barcelona aliyemudu kupiga shuti lililokwenda langoni mwa wapinzani katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa San Siro lakini bado anajiamini kuwa kikosi hicho kinaweza kumudu kutotolewa katika hatua ya timu 16 bora kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Xavi anakiri kuwa hawakucheza vizuri katika mchezo huo kwasababu hawakutumia vyema nafasi za upande wa pembani zilizokuwepo na pia kushindwa kujaribu mashuti ya mbali lakini anadhani wanaweza kufanyia kazi makosa yaliyojitokeza na kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo wao marudiano. Maandalizi ya Barcelona katika mchezo wao wa ligi dhidi ya Sevilla mwishoni mwa wiki hii yanaonekana kuwa magumu zaidi kwa ukweli kwamba wanakabiliwa na mchezo wa marudiano ya Kombe la Mfalme dhidi ya Real Madrid Jumanne inayokuja.

No comments:

Post a Comment