Wednesday, February 20, 2013

MARADONA ATAMANI MWANAE ACHEZE ARGENTINA.

NGULI wa soka wa zamani wa kimataifa kutoka Argentina ameelezea ndoto zake za kumuona mwanae wa kiume aliyezaliwa karibuni Diego Fernando akiichezea nchi hiyo sambamba na watoto wa Lionel Messi na Sergio Aguero. Mpenzi wa zamani wa Maradona Victoria Ojeda alijifungua mtoto huyo mwishoni mwa wiki iliyopita huko jijini Buenos Aires wakati mtoto wa Messi aitwaye Thiago amefikisha miezi mitatu na nusu huku mtoto wa Aguero aitwaye Benjamin ametimiza miaka minne. Maradona aliiambia radio moja nchini Dubai kwamba ana ndoto kuona watoto hao wakiichezea Argentina siku huku akifafanua kuwa anadhani mtoto wa Messi atakuwa katika nafasi ya kiungo akiwalisha mipira Benjamini pamoja na Diego Fernando watakaokuwa wakicheza katika safu ya ushambuliaji. Maradona ambaye ni babu wa Benjamini Aguero amesema mapema wakati majukumu yake ya kibiashara yatakapomalizika atasafiri kwenda Argentina kumuona mwanae huyo aliyezaliwa. Nyota huyo ambaye ana mkataba jijini Dubai pia ana watoto wawili wa kike Dalma na Giannina ambao alizaa na mke wake wa zamani Claudia Villafane.

No comments:

Post a Comment