Wednesday, February 20, 2013

TEKNOLOGIA YA KOMPYUTA KUTUMIKA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limethibitisha kuwa mfumo wa teknologia ya kompyuta katika mstari wa goli unatarajiwa kutumika katika michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Brazil 2014. Mfumo huo ulitumika kwa mafanikio katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia iliyofanyika Desemba mwaka jana na pia itatumika katika michuano ya Kombe la Shirikisho itakayofanyika Juni mwaka huu. Rais wa FIFA mara kwa mara amekuwa akipigia debe mfumo huo toka alipoona bao halali alilofunga kiungo wa Uingereza Frank Lampard likikataliwa na kupelekea nchi hiyo kufungwa na Ujerumani katika michuano ya Kombe la Dunia 2010. FIFA katika mkutano wake wa mwaka jana ilipitisha mifumo miwili ya Goalref na Hawkeye ambayo yote kwa pamoja ilitumika katika michuano ya klabu bingwa ya dunia.

No comments:

Post a Comment