Tuesday, February 19, 2013

PISTORIUS AKIRI KUMPIGA RISASI MPENZIWE.

MWANARIADHA mlemavu Oscar Pistorius ametoa maelezo ya kuogofya kuhusu usiku aliompiga risasi rafiki yake wa kike na kumuua akidai kuwa alidhani ni mwizi wakati alipoamka katikati ya usiku wa manane. Katika taarifa iliyosomwa mbele ya mahakimu wa mahakama ya jijini Pretoria, mwanariadha huyo alidai kuwa alikuwa upande wa juu wa nyumba yake wakati aliposikia kelele kutoka bafuni. Taarifa hiyo iliendelea kusema kuwa Pistorius akiamini kuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp bado yuko kitandani kalala alichukua bastola yake na kupiga kelele kutoa onyo kabla ya kufyatua risasi nne kupitia mlangoni. Baada ya kufyatua risasi ndipo Pistorius anadai aligundua Steenkamp hakuwepo kitandani ikabidi akavunje mlango wa bafu hilo na kujaribu kumsaidia lakini alifia kwenye mikono yake. Pistorius ataendelea kubakia rumande mpaka kesi hiyo itakapoendelea tena leo baada ya mahakimu kuisimamisha kutokana na mtuhumiwa kushindwa kuwa katika hali yake ya kawaida.

No comments:

Post a Comment