Tuesday, March 26, 2013

SUPER EAGLE ITAFUZU KOMBE LA DUNIA - LAMOUCHI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Sabri Lamouchi anaamini kuwa timu ya taifa ya Nigeria-Super Eagles wanaweza kushinda kikwazo cha kutoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Kenya nyumbani na kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 itakayofanyika nchini Brazil. Nigeria mbao ni mabingwa wa Afrika walishindwa kutamba Jumamosi baada ya kupata sare katika dakika za lala salama kwa bao lililofungwa na mchezaji aliyetokea benchi Nnamdi Oduamadi lakini Lamouchi amedai kuwa atashangaa kama timu hiyo ikishindwa kwenda nchini Brazil. Kocha huyo amedai kuwa katika safari ya kuelekea nchini Brazil timu yake Ivory Coast lazima iwepo, timu nyingine moja au mbili kutoka Afrika ya Kaskazini, Nigeria na pengine Zambia anadhani ndio timu tano zitakazowakilisha bara la Afrika katika michuano hiyo. Nigeria iliitoa Ivory Coast katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Afcon iliyofanyika nchini Afrika Kusini na lamouchi anakiri kuwa hakutegemea kama timu hiyo ingetinga hatua ya nusu fainali mbele ya kikosi chake kilichosheheni nyota lukuki.

No comments:

Post a Comment