Friday, March 29, 2013

TEKNOLOJIA YA KOMPYUTA KATIKA MSTARI WA GOLI GHALI SANA - PLATINI.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA, Michel Platini amesema mfumo wa teknologia ya kompyuta kwenye mstari wa goli ni ghali sana kuutumia katika michuano ya Ligi ya Mabingwa. Platini amesema ni bora fedha hizo akazitumia katika kuinua soka la vijana na miundombinu kuliko kuzitumia kwa ajili ya kufunga mfumo huo. Platini aliongeza kuwa anafurahia uamuzi wa kutumia mfumo wa waamuzi watano katika Ligi ya Mabingwa na Europa League. Amesema gharama za kufunga mfumo huo katika viwanja 280 vinavyotumika kwa ajili ya michuano hiyo inafikia kiasi cha paundi milioni 46 katika kipindi cha miaka mitano hivyo anaona ni gharama kubwa sana kwa makosa ambayo yanaweza kufanyika mara moja katika kipindi cha miaka 40. Shirikisho la Soka Duniani-FIFA limepanga kutumia mfumo huo katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil. 

No comments:

Post a Comment