Sunday, April 28, 2013

BILBAO YAITIBULIA BARCELONA MIPANGO YA UBINGWA.

KLABU ya Barcelona inabidi isubiri wiki nyingine ili iweze kutangaza ubingwa wa Ligi Kuu nchini Hispania baada ya Athletico Bilbao kulazimisha sare ya mabao 2-2 Jana huku mahasimu wao Real Madrid nao wakijichimbia katika nafasi ya pili baada ya kuwafunga ndugu zao Atletico Madrid mabao 2-1. Ushindi wa Barcelona dhidi ya Bilbao na kama mahasimu wao Madrid wangefungwa katika mchezo wao ungeiongezea pengo la alama 16 Barcelona huku wakiwa wamebakiwa na mechi hivy moja kwa moja kutangazwa mabingwa wapya wa La Liga. Lakini kwa matokeo yalivyokuwa jana Barcelona bado wana mchezo mmoja zaidi ili waweze kutwaa ubingwa wa La Liga msimu huu. Barcelona ina kibarua kigumu Jumatano ijayo mbele ya Bayern Munich ambapo inatatakiwa kupata ushindi wa zaidi ya mabao manne ili iweze kukata tiketi ya kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kufungwa mabao 4-0 katika mchezo wa kwanza.

No comments:

Post a Comment