Sunday, April 28, 2013

LIVERPOOL WALIKUWA SAHIHI - FERGUSON.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson anaamini kuwa Liverpool walikuwa sahihi kutochukua hatua dhidi ya mshambuliaji wao Luis Suarez kabla ya kufungiwa mechi 10 na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa kumng’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic. Ferguson amesema tukio hilo linamkumbusha jinsi walivyotendwa na FA baada ya mshambuliaji wake Eric Cantona kumpiga teke la kung-fu mshabiki wa Crystal Palace mwaka 1995. Ferguson amedai kuwa FA iliwahakikishia kuwa hatachukua hatua zaidi kama United watamuadhibu mchezaji huyo lakini pamoja na United kumfungia Cantona miezi minne, chama hicho kiliongeza adhabu na kufikia miezi nane. Kwa matokeo hayo yaliyowakuta United kipindi hicho Ferguson amesema ameelewa kwanini Liverpool hawakumuadhibu nyota huyo mapema.

No comments:

Post a Comment