Saturday, April 27, 2013

NYOTA WA BIRMINGHAM MBARONI KWA KUSABABISHA AJALI.

POLISI nchini Uingereza wamebainisha kumkamata mshambuliaji mtukutu wa klabu ya Birmingham City Marlon King kwa tuhuma za uendeshaji hatarishi. King alishikiliwa na polisi kufuatia ajali iliyohusisha magari matatu katika kitongoji cha Nottinghamshire jana ajali ambayo ilipekekea mtu mmoja kujeruhiwa vibaya huku mchezaji huyo akiachiwa baadae kwa dhamana wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea. Msemaji wa klabu hiyo iliyopo ligi daraja pili amethibitisha kuwa na taarifa ya ajali ambayo imemhusisha mchezaji wao na kudai kuwa suala hilo bado linachunguzwa na polisi hivyo hawezi kuzungumzia zaidi. King alifanyiwa upasuaji wa mguu mwezi uliopita ambao utamfanya kukaa nje ya uwanja kwa msimu mzima.

No comments:

Post a Comment