Saturday, April 27, 2013

NEYMAR KUONDOKA SANTOS.

MAKAMU wa rais wa klabu ya Santos ya Brazil, Odilio Rodriguez amebainisha kuwa Neymar ameiambia klabu hiyo kuwa yuko tayari kuondoka kwenda timu nyingine na hatarajii kusaini mkataba mwingine. Mkataba wa mshambuliaji huyo nyota unatarajiwa kuisha katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka 2014 na Santos walikuwa na nia ya kumbakisha kinda huyo mpaka baada ya michuano ya Kombe la Dunia 2014. Hatahivyo, Neymar mwenye umri wa miaka 21 ameweka wazi kuwa muda wake wa kuwepo Santos unakaribia kufikia mwishoni ambapo anataka kwenda kuonyesha ujuzi wake mahali pengine. Rodriquez alithibitisha hilo na tayari vilabu mbalimbali vikubwa barani Ulaya vimekuwa vikipigana vikumbo kutaka sahihi ya nyota huyo.

No comments:

Post a Comment