Saturday, April 27, 2013

VILANOVA KUENDELEA KUINOA BARCELONA MSIMU UJAO.

KOCHA wa klabu ya Barcelona, Tito Vilanova ana nia ya kuendelea kuinoa klabu hiyo msimu ujao pamoja na athari za matibabu yake ya kansa ya koo na pia anaamini kuwa kikosi chake inaweza kuitoa Bayern Munich na kutinga fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akihojiwa katika mkutano wake wa kwanza na waandishi toka alipotoka katika matibabu ya mionzi jijini New York mwezi mmoja uliopita, Vilanova amesema bado ana shauku kubwa na kuendelea na kazi yake na hakuna mara moja alipofikiria kuacha. Vilanova amesema madaktari kuwa kitu kizuri cha kufanya kwasasa ili kumsaidia kupona ni kufanya kazi na anafurahia jambo hilo. Kocha huyo pia mbali na timu yake kugaragazwa na Bayern kwa mabao 4-0 Jumanne iliyopita lakini ameonyesha kujiamini kwamba wachezaji wake wanauwezo wa kugeuza matokeo katika mchezo wa marudiano utakaopigwa katika Uwanja wa Camp Nou Jumatano ijayo. Vilanova amesema anaamini wachezaji wake wanaweza kufanya maajabu katika mchezo huo haswa ikizingatiwa watakuwa wakicheza mbele ya mashabiki wao ingawa amekiri itakuwa kazi ngumu kwani wapinzania wao nao hawataifanya kazi yao iwe rahisi.

No comments:

Post a Comment