Sunday, April 28, 2013

ROONEY MCHEZAJI TAJIRI ZAIDI EPL.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Manchester United, Wayne Rooney ndio mchezaji mwenye fedha nyingi zaidi katika Ligi Kuu nchini humo akiwa na utajiri unaokadiriwa kufikia paundi milioni 51. Wachezaji 24 wa ligi kuu nchini humo ni miongoni mwa orodha ya wanamichezo 100 matajiri nchini Uingereza na Ireland. Utajiri wa Rooney umeongezeka kwa paundi milioni sita kwa mwaka jana na ukijumlisha na utajiri wa mkewe Coleen unafikia kiasi cha paundi milioni 64. Mchezaji mwenzake wa United Rio Ferdinand yeye yuko katika nafasi ya pili akiwa na utajiri unaofikia paundi milioni 42 wakati mshambuliaji wa Stoke City Michael Owen yuko katika nafasi ya tatu akiwa na kiasi cha paundi milioni 38. Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza, David Beckham ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa yeye anashika nafasi ya 11 katika wanamichezo matajiri duniani akiwa na utajiri unaofikia paundi milioni 165 ambapo nafasi ya kwanza katika orodha hiyo inashikiliwa na mcheza gofu Tiger Woods mwenye utajiri unaofikia paundi milioni 570.

No comments:

Post a Comment