Sunday, April 28, 2013

GIGGS ALINIPA TABU SANA KIPINDI NACHEZA - LAUREN.

BEKI wa zamani wa kimataifa wa Cameroon na klabu ya Arsenal Lauren Mayer amebainisha kuwa mshambuliaji wa Manchester United Ryan Giggs alikuwa akimpa wakati mgumu kumkaba wakati akicheza soka. Lauren ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha Arsenal ambacho kilimaliza msimu wa mwaka 2004 bila kufungwa katika Ligi Kuu nchini Uingereza yuko jijini Kampala kwa mwaliko wa mpango wa kuinua vipaji wa Airtel rising stars. Beki huyo nyota wa zamani pia alimtaja mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thierry Henry kama mmoja wa washambuliaji wagumu kuwakaba pindi walipokuwa mazoezini kwasababu ya kasi na ufundi wa hali ya juu aliokuwa nao. Lauren amesema wakati akicheza alipata wakati mgumu kumkaba Giggs kwasababu alikuwa mjanja sana na ilikuwa sio rahisi kugundua anachotaka kufanya awapo na mpira kama ilivyo kwa wachezaji wengine wa nafasi yake. Nyota huyo pia amesema kama ilivyo kwa mashabiki wengine wa Arsenal nay eye anachukizwa na kitendo cha timu hiyo kutoshinda taji lolote kwa kipindi kirefu lakini ana imani na kocha Arsene Wenger kwa mba atarekebisha hilo na mambo yatakuwa mazuri kipindi kifupi kijacho.

No comments:

Post a Comment