Tuesday, April 30, 2013

FERGUSON AKIRI MAPAMBANO MAKALI KATIKA USAJILI KIANGAZI.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amekiri atakuwa katika mapambano makubwa na mahasimu wake Manchester City na Chelsea mara dirisha la usajili majira ya kiangazi litakapofunguliwa. Pamoja na kutwaa taji la Ligi Kuu nchini Uingereza, Ferguson tayari ameanza kujipanga kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao na anatatarajia kusajili wachezaji nyota kadhaa. Ferguson atawaongeza nyota hao atakaowasajili katika majira ya kiangazi na kuwaunganisha na kikosi chake cha sasa ambacho kimesheheni wachezaji vijana kwa ajili ya kutetea taji lake la ligi na kujaribu kufika mbali katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Kocha huyo amesema ni lazima aongeze nguvu katika kikosi chake ili waongeze nguvu damu change alizonazo kwani wachezaji wenye umri mkubwa alionao tayari soka lao linelekea ukingoni hivyoni muhimu kufanya mabadiliko.

No comments:

Post a Comment