Tuesday, April 30, 2013

MWAMUZI AFUNGIWA MAISHA URUSI KWA KUSHAMBULIA.

MWAMUZI msaidizi wa ligi ya soka nchini Urusi amefungiwa maisha jana kufuatia kumshambulia mchezaji wa miaka 18. Mwamuzi huyo Musa Kadyrov alimshambulia beki wa timu ya Amkar Perm, Ilya Krichmar mara baada ya kupulizwa filimbi ya kumaliza mchezo kati ya timu hiyo na wenyeji Terek katika mji wa Grozny, Chechnya. Krichmar amesema mara baada ya mwamuzi wa kati kupuliza filimbi ya mwisho alianza kutembea kuelekea katika benchi lao la ufundi ndipo ghafla mwamuzi huyo alipokuja nyuma yake na kumsukuma kisha kuanza kumpiga mateke. Mchezaji anaendelea kusema muda mfupi baadae wachezaji wa timu mwenyeji nao walivamia eneo hilo na kuanza kumshambulia kabla ya wachezaji wenzake hawajafika na kumuokoa asiendelee kupata kichapo zaidi. Wadau wa masuala ya michezo huko Chechnya wameungana kuponda kitendo kilichofanywa na Kadyrov na kudai kuwa adhabu ya kufungiwa maisha kwa mamuzi huyo haikutosha kutokana na kitendo cha aibu alichofanya.

No comments:

Post a Comment