Monday, May 6, 2013

KAGAME KUANDALIWA DARFUR NA KORDOFAN YA KUSINI.

KATIBU Mkuu wa Baraza la Michezo kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA, Nicholas Musonye amesema wameteua miji Darfur na Kordofan ya Kusini nchini Sudan kuwa wenyeji wa michuano ya vilabu inayoandaliwa na baraza hilo. Musonye amesema michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kati ya June 18 na Julai 2 mwaka huu. Aliendelea kusema kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya kufanya ziara ya kukagua miundo mbinu pamoja na usalama katika miji hiyo ambayo imekabiliwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi kirefu sasa. Amesema viwanja walivyochagua ni Uwanja wa El Fasher uliopo jijini Darfur na uwanja mwingine mdogo wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 20,000 uliopo Kordofan ya Kusini. Vilabu 13 vimeshathibitisha kushiriki michuano hiyo wakiwemo Yanga ya Tanzania ambao ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment