Tuesday, May 28, 2013

NEYMAR AMWAGA WINO RASMI BARCELONA.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Brazil, Neymar ametanabaisha kuwa sasa yeye ni mchezaji rasmi wa klabu ya Barcelona ya Hispania. Neymar amesema amesaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo jana, zikiwa zimepita siku mbili baada ya kutangaza kuwa ameamua kuchagua timu hiyo badala ya mahasimu wao Real Madrid. Nyota amesema anaondoka Santos huku akiwa na majonzi lakini pia ni heshima kwake kusajiliwa na klabu kama Barcelona na kupata nafasi ya kucheza na baadhi ya wachezaji bora kabisa duniani. Neymar mwenye umri wa miaka 21 atajiunga na nyota wenzake Barcelna akiwemo mshindi wan ne mfululizo wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia Lionel Messi, Xavi Hernandez na Andres Iniesta. Sio Neymar wala Barcelona walioweka wazi ada halisi ya uhamisho huo lakini vyombo vya habari nchini Brazil vimedai kuwa Barcelona watalipa kiasi cha euro milioni 30 kwa nyota huyo.

No comments:

Post a Comment