Tuesday, June 25, 2013

ANCELOTTI ACHUKUA MIKOBA YA MOURINHO MADRID.

KLABU ya Real Madrid imemtangaza rasmi Carlo Ancelotti raia wa Italia kuwa kocha mpya wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu. Kocha huyo wa zamani wa klabu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa atatangazwa rasmi mbele ya waandishi wa habari Jumatano kuchukua nafasi ya Jose Mourinho aliyekwenda kufundisha klabu yake ya zamani ya Chelsea. Katika mtandao wa wake klabu hiyo imedai kufikia hatua hiyo kutokana na uzoefu wa Ancelotti wa kukabiliana na changamoto mbalimbali katika vilabu vikubwa kama Juventus, AC Milan, Chelsea na PSG. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 54 amekuwa akihusishwa kwenda Madrid toka Mourinho alipoondoka lakini alishindwa kuondoka mpaka PSG walipopata mbadala wake ambaye ni kocha wa zamani wa Ufaransa Laurent Blanc. Vyombo vya habari nchini Hispania vimedai Madrid wamelazimika kuilipa PSG euro milioni 4 kama kifuta jasho kwasababu Ancelotti alikuwa amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake kwenye klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment