Tuesday, June 25, 2013

KUTOLEWA KWANGU SIO JAMBO LA KUTISHA - NADAL.

BINGWA wa michuano ya wazi ya Ufaransa, Rafael Nadal amedai kuwa kutolewa kwake katika mzunguko wa kwanza wa michuano ya Wimbledon kwa kufungwa na Steve Darcis sio jambo kubwa na kukataa kulaumu kutoka kwake kumetokana na majeruhi ya kifundo cha mguu ambayo yamemuweka nje kwa kipindi kirefu. Akihojiwa Nadal ambaye amewahi kunyakuwa michuano ya Wimbledon mara mbili amekiri kutolewa mapema katika michuano ni jambo gumu lakini kama limetokea haina jinsi kwani maisha yanaendelea. Nadal alimsifu mpinzani wake kwa kucheza vizuri na kushindwa kupata nafasi ya kucheza anavyotaka na kwasasa anaenda nyumbani kujipanga kuangalia alikosea wapi ili ajipange kwa ajili ya michuano ijayo. Kutolewa kwa Nadal kunampa ahueni Andy Murray wa Uingereza kusafishiwa njia ya kwenda mpaka fainali ya michuano hiyo kwasababu walikuwa wamepangwa kundi moja.

No comments:

Post a Comment