Wednesday, June 26, 2013

FIFA YAWASHUSHIA NYUNDO WAAMUZI WALIOKUTWA NA HATIA YA KUPEWA RUSHWA YA NGONO ILI WAPANDE MATOKEO.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limewapiga marufuku waamuzi wasaidizi wa Lebanon kuchezesha mechi za soka popote duniani ambao wamefungwa jela nchini Singapore kwa kukubali rushwa ya ngono ili wapange matokeo. Ali Eid na Abdallah Taleb tayari walikuwa wamefungiwa na Shirikisho la Soka la Asia-AFF huku kesi yao ikisikilizwa na sasa FIFA nao wameongeza adhabu hiyo na kuwa dunia nzima. Wawili hao walihukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela Juni 10 kwenye kesi hiyo iliyoanza kusikilizwa April 4 mwaka huu huku mwamuzi Ali Sabbagh yeye akifungwa miezi sita siku iliyofuata. Waamuzi hao watatu walikuwa wamepangwa kuchezesha mechi ya AFF kati ya Tampines Rovers ya Singapore na East Bengal ya India mwezi April lakini walibadilishwa muda mchache kabla ya kuanza kwa mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment