Thursday, June 20, 2013

BLAKE KUTOSHIRIKI MBIO ZA DUNIA ZA MITA 200.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Yohan Blake anatarajiwa kutoshiriki mashindano ya dunia yam bio za mita 200 baada ya kujitoa katika mbio za kufuzu zitakazofanyika mwishoni mwa wiki hii kwasababu ya kusumbulia na msuli. Blake mwenye umri wa miaka 23 alikumbwa na majeraha hayo April mwaka huu na mpaka sasa bado hajapona sawasawa. Akiwa kama bingwa mtetezi wa mbio za mita 100 zitakazofanyika jijini Moscow, Blake hatahitajika kukimbia mbio za mchujo. Mwanariadha mwenzake Usain Bolt yeye tayari ameshavuzu moja kwa moja mbio za mita 200 kwakuwa ndio bingwa mtetezi lakini atalazimika kukimbia mbio za mchujo za mita 100 baada ya kuenguliwa katika michuano ya dunia ya mbio hizo kwa kudanganya jijini Daegu mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment