Thursday, June 20, 2013

NEYMAR AUNGA MKONO MAANDAMANO YA BRAZIL.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Brazil, amejiunga na wachezaji wenzie wa timu ya taifa ya nchi kuunga mkono maandamano yanayoendelea nchi nzima na kuikosoa serikali ya rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff kwa kushindwa kutoa huduma za kijamii za kutosha. Neymar aliandika katika mtandao wake wa kijamii saa chache kabla ya Brazil haijachuana na Mexico katika mechi yao ya pili ya Kombe la Shirikisho akidai kuwa nasikitishwa na kinachoendelea nchini humo. Neymar aliendelea kuandika kuwa mara nyingi amekuwa na imani kwamba haina haja ya kuingia mtaani kuandamana ili kudai mazingira mazuri kwenye masuala ya usafiri, afya, elimu na usalama kwakuwa suala hilo ni jukumu la serikali. Nchi hiyo imekuwa ikikumbwa na maandamano makubwa wiki hii juu ya dola bilioni tano zilizotumika kwa ajili ya kuandaa michuano ya Kombe la Shirikisho na Kombe la Dunia litakalofanyika mwaka ujao wakati hakuna fedha fedha zozote zilizotengwa kwa ajili ya kuendeleza elimu na afya. Waandamanaji hao pia wamekuwa wakipinga nauli kubwa kwenye vyombo vya usafirishaji kwa kudai kuwa hatua ya kufanya hivyo ni ufisadi.

No comments:

Post a Comment