Tuesday, June 25, 2013

SHIRIKISHO LA SOKA LA ETHIOPIA LAMTOA KAFARA KATIBU MKUU WAKE.

SHIRIKISHO la Soka la Ethiopia-EFF limemtimua kibarua katibu mkuu wake wake baada ya kukiri kumtumia mchezaji kimakosa katika mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 hatua ambayo inaweza kuigharimu timu nchi hiyo kukatwa alama tatu. Kamati ya Utendaji ya EFF ilipiga kura za kumtimua katibu huyo aitwaye Ashenafi Ejigu lakini walipinga barua ya kujiuzulu kwa makamu wa rais wa shirikisho hilo Berhanu Kebede ambaye ndiye alikuwa akilaumiwa kutokana na mkanganyiko huo. Baadhi ya wajumbe na waandishi wa habari za michezo waliokuwepo katika mkutano huo walikuwa wakitaka uongozi mzima wa shirikisho hilo ujiuzulu kwa kile walichokiita uzembe. Rais wa EFF, Sahilu Gebremariam alikiri kuwa suala hilo ni la kizembe na wanapaswa wote kujiuzulu na kudai kuwa atafanya hivyo katika mkutano mkuu utakaofanyika Septemba mwaka huu. Akihojiwa kuhusiana na suala la kumchezasha mchezaji aliyepewa kadi mbili za njano kocha wa Ethiopia Sewnet Bishaw alijitetea kuwa anapokuwa uwanjani huwa hatumii karatasi na kalamu anachofanya yeye ni kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri.

No comments:

Post a Comment