Wednesday, July 31, 2013

BARCELONA YAMPOTEZA NGULI WAKE WA ZAMANI.

KLABU ya Barcelona imetangaza katika mtandao wake kumpoteza mchezaji wake wa zamani Antoni Ramallets aliyefariki dunia Jumanne akiwa na umri wa miaka 89. Ramallets ambaye alikuwa golikipa aliichezea Barcelona mechi 400 kati ya mwaka 1946 na 1961, na kuisaidia timu hiyo kushinda mataji sita ya La Liga na mataji mengine matano ya Kombe la Mfalme. Rais wa Barcelona, Sandro Rosell alikaririwa na mtandao huo akitoa salamu zake za rambirambi kwa kumuelezea Ramallets kama mmoja wa makipa bora waliowahi kuichezea klabu hiyo hivyo siku ya jana ilikuwa siku ya masikitiko makubwa kwao kumpoteza. Wachezaji wa Barcelona walisimama kwa dakika moja katika mchezo wao wa kirafiki wa Jumanne dhidi ya Lechia Gdansk ili kumkumbuka golikipa huyo wa kimataifa wa Hispania.

No comments:

Post a Comment