Monday, August 26, 2013

CAF YAZIRUHUSU ZAMALEK NA AL AHLI KUCHEZA MECHI ZAO NYUMBANI PAMOJA NA MACHAFUKO.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limedai kuwa mechi mbili za Ligi ya Mabingwa ya Afrika zitafanyika nchini Misri kama zilivyopangwa pamoja na machafuko yanayoendelea ambayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,000 toka jeshi litwae madaraka mwezi uliopita. Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika mtandao wa CAF mabingwa watetezi wa michuano hiyo Al Ahli itacheza na AC Leopards ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-DRC katika Uwanja wa El Gouna na kufuatiwa na mechi kati ya Zamalek na Orlando Pirates ya Afrika Kusini mechi zote zitachezwa mwishoni mwa wiki ijayo. Klabu hizo mbili maarufu nchini Misri ambazo zimekuwa zikitawala soka la Afrika katika kipindi cha karibuni zote zimepangwa katika kundi A ambalo Pirates ndio wanaoongoza wakiwa na alama saba. Ahli wanafuatia katika nafasi ya pili wakiwa na alama nne sawa na Leopards waliopo nafasi ya tatu huku Zamalek wakishika mkia katika kundi hilo wakiwa na alama moja. Mechi zote mbili zitachezwa bila mashabiki baada ya mamlaka husika kuepuka mikusanyiko ambayo inaweza kuzua machafuko zaidi.

No comments:

Post a Comment