Monday, August 26, 2013

TOTTENHAM WAKUBALI KUMWACHIA BALE KWA PAUNDI MILIONI 86.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Wales, Gareth Bale yuko huru kujiunga na Real Madrid baada ya Tottenham Hotspurs kukubali uhamisho wa rekodi wa paundi milioni 86 Jana usiku. Usajili huo wa Bale kwenda Madrid utavunja rekodi ya duniani ya usajili wa paundi milioni 80 ambao klabu hiyo iliipa Manchester United kwa ajili ya Cristiano Ronaldo mwaka 2009. Inaaminika kuwa safari ya mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy kwenda Madrid kukutana na Perez ilikuwa ni moja ya mbinu za kiongozi huyo ili aweze kumuuza nyota huyo kwa bei ghali zaidi. Mbali na Spurs kufaidika kwa kumuuza Bale ambaye walimnunua kwa paundi milioni saba kutoka Southampton miaka sita iliyopita pia mchezaji huyo anatarajiwa kukunja kitita cha paundi 300,000 kwa wiki katika mkataba wa miaka sita anaotarajiwa kusaini.

No comments:

Post a Comment