Sunday, August 25, 2013

CHELSEA YATHIBITISHA KUFIKIA MAKUBALIANO NA WILLIAN PAMOJA NA ANZHI KUHUSU UHAMISHO WA KIUNGO HUYO.

KLABU ya Chelsea imebainisha kufikia makubaliano na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi pamoja na kiungo Willian kwa ajili ya uhamisho wa kutua Stamford Bridge. Kiungo huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 25 alionekana atasajili Tottenham Hotspurs baada ya kufanyiwa vipimo vya afya Alhamisi iliyopita lakini Chelsea waliwapiga bao baada ya kuongeza dau. Willian alisafiri kwenda Uingereza wiki iliyopita akitegemewa kusajili Spurs ili kuziba nafasi ya Gareth Bale baada ya mchezaji huyo pia kufanya mazungumzo na Liverpool. Pamoja na kufanyiwa vipimo vya afya katika uwanja wa mazoezi wa Spurs lakini nyota huyo alidai kuwa alikuwa akitafuta timu inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa ndio maana haikuwa ngumu kwake kubadili mawazo Chelsea walipomfuata na dau kubwa.


No comments:

Post a Comment