Sunday, August 25, 2013

NEYMAR KUANZA KWA MARA YA KWANZA KATIKA KIKOSI CHA BARCELONA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Barcelona, Neymar anatarajiwa kwa mara ya kwanza kupangwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo kitakachocheza na Malaga wakati Lionel Messi akikosa mchezo huo kutokana na majeruhi aliyopata katika mechi ya Super Cup dhidi ya Atletico Madrid Alhamisi iliyopita. Neymar ambaye alisajili kwa euro milioni 57 mapema katika kipindi hiki cha usajili wa majira ya kiangazi akitokea Santos alipoteza kilo saba kufuatia upasuaji wa kuondoa mafindofindo baada ya michuano ya Kombe la Shirikisho Juni mwaka huu na amekuwa akipambana ili kurejea katika kiwango chake toka wakati huo. Neymar ambaye alianzia katika benchi la wachezaji wa akiba katika ushindi wa mabao 7-0 katika mechi ya La Liga dhidi ya Levante na kufunga bao lake kwanza akiwa na timu hiyo wakati alipoisawazishia katika sare ya bao 1-1 waliyopata dhidi ya Atletico. Meneja wa Barcelona, Gerard Martino alidai wiki iliyopita hawataki kumuwekea shinikizo lolote nyota wao huyo kwani wanataka azoee kucheza na wenzake kidogo kidogo.

No comments:

Post a Comment